Lord Eyez azungumzia ujio wake mpya baada ya kurudishwa Weusi - COW BOY BISHOO

Breaking

Monday, 18 August 2014

Lord Eyez azungumzia ujio wake mpya baada ya kurudishwa Weusi

Rapper wa kundi la Nako 2 Nako Soldiers na member wa kampuni ya Weusi, anatarajia kurejea tena hewani hivi karibuni baada ya kumaliza tofauti zake na uongozi wa Weusi.
Miezi kadhaa iliyopita, rapper huyo alisimamishwa kwenye kampuni ya Weusi kutokana na kukiuka maadili kwa kushutumiwa kuhusika katika tukio la wizi. Rapper huyo amesema mashabiki wake watarajie ngoma yake mpya iliyotayarishwa na producer wa B Records, Chizan Brain.
“Nina mawe kama manne hivi nimeshapika na maraia kibao lakini ngoma zangu,” amesema rapper huyo.
Hivi karibuni kupitia Kikaango cha East Africa TV, msemaji wa Weusi, Nicki wa Pili alithibitisha kurejeshwa kundini kwa Lord Eyez akisema kuwa katiba ya Weusi inasema watu watano ndio wanaounda kampuni hiyo.

No comments:

Post a Comment