Hii Kuhusu Dkt John Wa Wagosi Wa Kaya Kunusurika Kifo Baada Ya Kupata Ajali - COW BOY BISHOO

Breaking

Tuesday, 3 June 2014

Hii Kuhusu Dkt John Wa Wagosi Wa Kaya Kunusurika Kifo Baada Ya Kupata Ajali

Dkt John ameeleza kuwa alikuwa anaendesha pikipiki katika mitaa ya Tanga jana majira ya mchana kwa kuwa gari lake likuwa kwa fundi likibadilishwa bodi, lakini alikutana na gari dogo ambalo dereva wake alichelea kuzifuata sheria za barabarani na kusababisha ajali.
“Jamaa alikuwepo mbele yangu yeye hakuwasha endicator kama anakata kulia kuelekea kwenye ofisi ya Raha Leo, matokeo yake mimi nikajua ananyoosha atapita kwenye soko la Ngamiani. Mimi nikajichanganya kwenye 18, kumbe jamaa wala hanyooshi wala nini anakata bwana. Kwa hiyo akawa anakata halafu ndio anawasha indicator. Kwa hiyo akanipush…nikamvaa akanipush.”
Ameeleza kuwa alipata jeraha kubwa katika mguu wake wa kushoto bada ya kidonda kuchimbika nusra aguswe katika mfupa na ameshonwa nyuzi nane.
“Goti limevunjika kidogo, kwa hiyo kesho nategemea kupata transfer kwa ajili ya kuelekea Muhimbili ili nikatibiwe, kama itakuwa hivyo kwa sababu kuna daktari mmoja ndio tunaemsubiria, kama atakuwa hajarudi itabidi nikatibiwe Muhimbili kama wiki sita hivi.”

No comments:

Post a Comment