Wapiganaji wa Boko Haram wanataka kutawala eneo la Kaskazini mwa Nigera kwa kutumia sheria ya kiisilamu. Inaripotiwa
kuwa wanawake pamoja na wasichana sitini walitekwa nyara Kaskazini
Mashariki mwa Nigeria wiki iliyopita.Ripoti zilizotolewa mwishooni mwa
wiki iliyopita zilisema kuwa ishirini kati yao walichukuliwa na kundi
linaloaminika kuwa Boko Haram.
Serikali ya Nigeria imekuwa ikishinikizwa kuwanusuru waliotekwa nyara eneo la Chibok, Sio
jambo la kushangaza kwamba tangu kutekwa nyara kwa wasichana miambili
wa shule kutoka Chibok , wanawake wengine wametekwa nyara. Vijiji
vingi katika eneo la Kaskazini mwa Nigeria, vinakumbwa na utovu wa
usalama na wakati ambapo Boko Haram wanapofanya shambulizi,wao huchukua
muda mrefu wakifanya uporaji na mauaji.
Mwishoni mwa wiki, idadi kubwa ya watu waliuawa karibu na eneo la Chibok.
Zaidi ya wasichana 200 wa shule walitekwa nyara eneo la Chibok mwezi Aprili
Walitekwa nyara kutoka shule yao ya mabweni na wapiganaji wa Boko Haram.
Serikali ya Nigeria imekuwa chini ya shinikizo kali za kuitaka ifanye jitihada za kuwaokoa wasichana hao.Wanawake
hao walitekwa wakati wa uvamizi uliofanywa katika vijiji vilivyo katika
wilaya ya Damboa katika jimbo la Borno.Wanawake hao inaarifiwa
walitekwa nyara katika eneo la vijijini ambakop mawasiliano ni magumu
sana , sababu ya kupata habari hizi kuchelewa. Watu wanaotoroka vijiji ambavyo vilishambuliwa, wanasema kuwa wanawake na wasichana sitini walitekwa nyara wiki jana.
Baadhi ya watoto
waliotekwa ni wadogo sana wa umri. Moja ya vijiji vilivyoshambuliwa ni
kile cha Kummabza kilicho katika eneo la Damboa katika jimbo la Borno. Hata
hivyo haijaweza kuthibitisha idadi kamili ya watu waliotekwa nyara.
Hali hii imefanywa kuwa ngumu'kwani maafisa wa eneo hilo bado hawajatoa
tamko lolote kuhusu kisa hiki labda kutokana na hofu juu ya maisha yao. TOA MAONI APO CHINI


No comments:
Post a Comment