News:Baada ya Fanani kuachana na matumizi ya madawa ya kulevya, Prof Jay kurudisha kundi la Hard Blasters - COW BOY BISHOO

Breaking

Tuesday 30 September 2014

News:Baada ya Fanani kuachana na matumizi ya madawa ya kulevya, Prof Jay kurudisha kundi la Hard Blasters

Lile kundi la Hiphop lilikua linaundwa na Heavy Weight MC, Profesa Jay, Big Wille pamoja na Fanani, "Hard Blasters" ambao walikua active kuanzia miaka ya tisini hadi miaka ya 2000 mwanzoni, baada ya kuachia album iliyokuwa na ngoma kali na hit kama chemsha bongo na niamini, na kupotea kwenye ramani baada ya hapo,
sasa kundi hilo (HBC) linatarajiwa kurudi tena kwenye ramani ya bongo fleva chini ya studio za Mwanalizombe zinazomilikiwa na Prof Jay.

 "Hard Blasters kipindi kirefu, kila mtu aliamua kuishi maisha yake, mi nilipoamua kuwamba kufanya solo project kwasababu wenzangu waliokuwa slow kidogo, na mimi kwasababu niliamua muziki uwe maisha yangu, ndio kazi yangu na ndio maana niliacha kazi niliyoajiriwa ili nifanye mziki, ilibidi niendelee kufanya mziki, nilishindwa kuwasubiri wenzangu, lakini kwasababu wako tayari na wako pamoja na bado tunaishi pamoja, kila siku ilikuwa nikiwauliza lini wanaweza wakawa tayari wanasema tutafanya tutafanya tutafanya, lakini kila kitu kinatokea kwasababu, so the time is now naona, watu wakae tayari tu, chamsingi watu wakae tayari tu kwa Hard Blasters". Jay

No comments:

Post a Comment